Tuesday 9 December 2014

JINSI YA KUPATA MAPENZI UNAYOTAKA KATIKA NDOA.

   Mkiwa kwenye uhusiano,ni suala la msingi sana kujua namna ya kufanya ili kupeana raha,kwa sababu hakuna mtu anayeingia kwenye ndoa kusaka mtu wa kumtukana matusi au kumpiga.
Wako wanaume ni madikteta,anamburuza mke kadri anavyotaka,wala hajali hisia zake,kitu ambacho ni kibaya.Kuna wanaume wanafikiri wanawake ni kama gunia,unamfanyia vituko na matusi unavyotaka,unamnyanyasa na kumsema kwa watu kadri unavyotaka,kitu ambacho si sawa,kuna wanaume wengine licha ya kutanbuliwa kama vichwa vya nyumba,akikwaruzana na mwenzi wake,anachokijua ni kununa,kususa au hata kulala sebuleni,hii ni akili ya kitoto.
Mume kama kichwa cha nyumba,kinapaswa kuwa mfano wa kuigwa.Kila mwanaume anapaswa kujiangalia matendo yake.Lakini pia kila mwanamke anapaswa kuangalia  matendo yake anayofanya kwa ndoa yake na kwa mumewe.Je, ni matendo ya haki? Kila mwenye akili timamu anapaswa kufanya vitu ambavyo yeye akifanyiwa,atajihisi kupata raha.
Wakati mwingine tunakuwa na ndoa mbaya kwa sababu ya matendo tunayotenda.Ni lazima uwe makini kwa vitu ambavyo unafanya.Lakini ni muhimu katika uhusiano kuwa na kawaida ya kuwa na muda wa kutafakari kwa umakini mkubwa hali ya ndoa yako na kuona ni yapi yanakwenda hovyo au yanakwenda safi.Katika maisha msingi wa kuwa na maendeleo mema ni kuwaza na kufanya mema,ndio kusena hata kama labda ndoa yako ina matatizo,unapaswa kuwaza namna ya kufanya mema kwa maana ya kuondoa kasoro zilizoko na kadhalika.
Ni ujinga kutarajia mazuri kwenye ndoa yako wakati hufanyi mazuri,Ni  suala lisilowezekana,Utakuta mwanaume au mwanamke ni jeuri,lakini bado anatarajia maisha yake yawe na faraja,kitu kisichowezekana.Ni ujinga kukimbilia mwanamke au mwanaume mwingine na kuiacha ndoa yako,kwa sababu hakuna ambaye hana kasoro.Kama unafikiri yupo mwanamke au mwanaume ambaye hana kasoro,jua kuwa fikra zako haziko sawa.Kwa ufupi ni kwamba katika kila ndoa,kuna wakati kunatokea hitilafu,cha msingi ni kukaa chini na kuondoa kile ambacho kinaleta shida.
Cha msingi ni kwa watu kuacha dharau,kuacha majivuno,kuacha kuona kwamba  aaah nikimuomba msamaha ataona najikomba,hakuna ubaya kuitwa unajikomba ikiwa unachokitaka ni kizuri kwa ndoa yako.

No comments:

Post a Comment