Monday, 18 January 2016

KUMALIZA SHUGHULI HARAKA..(2)

Kawaida baada ya mwanaume kuwa na tabia ya kumaliza haraka kinachofuata ni kuanza kukwepa sex kitu ambacho inakuwa ngumu zaidi kudhibiti tatizo, mwanaume akiwa anauwezo wa kudhibiti kumaliza mapema pia huweza kuwa na hamu zaidi ya kufanya mapenzi.

Wengine hutumia njia ya kuondoa mawazo kujihusisha na tendo lenyewe kwa kuwaza vitu vingine hata hivyo hapo ni kujinyima raha na huweza kupelekea vitu kuwa ovyo zaidi.
Si vema kuhamisha mawazo yako kutoka kwenye akili zako wakati wa tendo la ndoa kwani ni sex muunganiko wa roho, mwili na nafsi.
Jambo la msingi ni kuwa na ufahamu wa viwango tofauti vya msisimko wa kimapenzi kuhusiana na kiungo chako (uume).
Unatakiwa kujua ni namna gani unajisikia unapokaribia kufikia hatua ambayo hakuna kurudi nyuma.

Ukishakuwa umefahamu unavyojisikia kuelekea point of No return hapo haitakuwa vigumu kufanya marekebisho ambayo yatakuruhusu kubaki umesisimka lakini bila kumaliza (kukojoa).

Kusisimka kimapenzi huwa ni mzunguka wa hatua 4 muhimu ambazo ni:-

KUPANDA KWA MDADI.
Huu ni wakati ambao kupumua huongezeka, uume husimama (hudinda). hatua ya pili ni:-

KILIMANI- hii ni hatua ambayo uume huwa umebaki umesisimka kwa kiwango cha juu.
Hatua inayofuata ni hatua ya tatu ambayo ni:-

KUMALIZA au KUKOJOA na hatua ya mwisho ambayo kupumua hurudi kama kawaida na uume hurudi na kuwa kawaida.
Ufunguo muhimu katika kudhibiti kumaliza mapema ni ku-maintain hatua ya pili yaani kubaki hapo kilimani bila kupiga risasi hata kama umelenga vizuri na unajisikia kuachia, hapa ndipo panahitaji imani na kujikana maana huwa ni kuelekea kwenye raha kamili ya sex kwa mwanaume, ila kumbuka uliye naye anahitaji uendelee zaidi.

NINI KIFANYIKE KUDHIBITI HALI HII?
Usitumie drugs au kilevi eti ndo unaweza kudhibiti hii hali, vitu kama hivi huweza kukupa interference na kupunguza uwezo wa kuelewa wakati muhimu wa wewe kuthibiti kumaliza mapema.
Kwanza jikubali, wanaume wengi huamini kwamba sex ni kwenye uume tu na pia kufanya mapenzi ni pale uume ukiingia kwenye uke tu.
Kufikiria hivyo ni tiketi ya moja kwa moja ya mwanaume kuwahi kukojoa au kumaliza.

Kufanya mapenzi kunakoridhisha (best sex) ni pamoja na kupeana mahaba, romance kuanzia juu kichwani kwenye nywele hadi kwenye kucha za vidole miguuni.
Mwanaume anayejifunza kujipa raha kimapenzi kupitia sehemu zote zinazompa raha (chuchu, lips, shingo, midomo, ulimi, nk) huweza kurelease tension kupitia hizo sehemu na kutosubiri sehemu moja tu yaani uume ndo iwe sehemu ya kupata raha ndo maana huweza kukojoa mapema.
Ni kwamba mwanaume anakuwa amefunga outlet zingine na kubaki na uume tu hivyo ni rahisi kufikia point ya no return tena kwa haraka mno.
Ukishajifunza kupata raha ya mapenzi kuanzia nywele kichwani hadi kucha miguuni maana yake mwili mzima unachukua raha ya mapenzi badala ya uume peke yake na matokeo yake utabaki ndani ya mke wako kwa muda mrefu.

Kujipa raha ya mapenzi ya mwili mzima ni njia ya ku-relax na kurelax ni moja ya njia muhimu za kujipa good sex.
Kwa mfano kuoga pamoja kwanza au kufanyiana massage kwanza kabla ya kuanza kwa tendo la ndoa husaidia mwanaume kurelax na zaidi kuupa mwili mzima sexual pleassure matokeo yake ni kufanya mapenzi kwa muda unaotosha na bibie kuridhika.

Kuwa na uwezo wa kupumua vizuri (deep breath) hii haina maana kwamba wakati unafanya mapenzi huwa hupumui, la hasha bali upumuaji wako inawezekana si ule usiotakiwa kwani wanaume wengi huzuia kupumua wakiwa kwenye sex.
Wengine huogopa kusikika wanapumua tofauti, sex ni kazi kama kazi zingine sasa usipopumua unadhani kitatokea nini, ikiwezekana pumua huku unatoa visauti, achia kupumua usijivunge kwani unapoficha kupumua maana yake unakaribisha uume ukusaidie kupumua na njia sahihi kwa uume kupumua ni kukojoa mapema.
Wengi baada ya kujifunza kupumua kwa kujiachia wamefanya mabadiliko makubwa sana katika muda wa kuwa ndani bila kumimina risasi.
· .
Ukishajua kuutumia mwili mzima kuhusika na raha ya mapenzi pamoja na kupumua sasa inakuja technic nyingine ya kujipiga stop.
Unaweza kuwasiliana na partner wako jinsi ya kupeana signal kwamba nakaribia kile kituo ambacho nikifika sitarudi tena, hakuna break.
Unaweza kutoa uume nje huku ukiendelea kupumua na ukiona unapata zile feelings kwamba huwezi kukojoa basi unaweza kurudi na kuendelea tena, kiasi cha kujipiga stop na kuendelea ni uamuzi wa ninyi wawili mnaohusika hasa baada ya mke kuridhika.

Kwa wale ambao kufanya mapenzi kupo katika level nyingine (oral sex) wanaweza kutumia oral sex kuthibiti mwanaume kumaliza mapema kwa mwanaume kujipa stop akiona anakaribia kumaliza kwa oral sex hii ni baada ya kupata mafanikio hasa baada ya kuona sasa mwanaume anaweza kwenda mbali zaidi ya kawaida yake.

Pia aina ya milalo wakati wa mapenzi huchangia mwanaume kumaliza mapema, kwa mfano missionary position (mwanaume juu mwanamke chini) huu huwezesha mwanaume kumaliza haraka kuliko mwanamke kuwa juu na mwanaume chini, otherwise mwanaume ni vizuri ukafanya utafiti wako kujua ni mlalo gani huwa unajisikia kuchelewa kumaliza na mke wako kuwahi kufika kileleni.

Pia ni vizuri kufanya mapenzi bila kuwa mabubu,kufanya mapenzi huku mnaongea husaidia mwanaume kurelax (na mwanamke pia) na husaidia mwanaume kuchukua muda mrefu kumaliza
Kujifunza kuthibiti kumaliza mapema kunaweza kuchukua muda mrefu na mazoezi ya kutosha, unaweza kujisikia kusumbuka tu wakati unajitahidi kuthibiti hata hivyo kwenye nia njia ipo na wewe utaweza tu nakuamini.

Mwisho, kujifunza mwanaume kumaliza mapema kutampa mpenzi wako raha kubwa sana kimapenzi. Wanawake hupenda good sex ambayo ni leisure, playful, whole body, massage kwa wingi.
Na wanawake wengi hulalamika kwamba wanaume huwa na haraka tukiwa kwenye miili yao, tupo too much mechanical, tunakimbilia kule chini tuingize tumalize na tuishie zetu kwa usingizi, tuna focus matiti na maeneo ya uke tu.
Wanawake hujisikia mwili mzima ni uwanja wa kucheza kimapenzi na hushangazwa na wanaume kugundua visehemu kidogo tu katika uwanja mzima na kuvipenda.
Hata uume pia umeumbwa kwa ajili ya leisure, kuchezewa, mapenzi ya mwili mzima, massage ya mwili mazima ndipo sex, kuwa focused kwenye uume peke yake huweza kuupa uume mgandamizo ambao hupelekea kutoa risasi mapema.

Kimsingi kama wanaume wangekuwa wanafanya mapenzi kwa namna ambayo wanawake wanapenda basi kusingekuwa na malalamiko na wanaume wangekuwa na matatizo kidogo yanayohusiana na tendo la ndoa.

KUMALIZA SHUGHULI HARAKA.

Baada ya kupeana mabusu na romance hadi kila mmoja anakuwa amesisimka kiasi cha kuwa tayari kwa kurushwa hadi kufika kileleni, ghafla baada ya msuguano mmoja tu mwanaume ameshamaliza na tayari hoi anageuka na kulala zake usingizi mzito wakati huohuo bibie bado kwanza ndo alianza kupata raha na sasa ameachwa kwenye mataa anazubaa akiugulia kukosa raha yenyewe.

Jambo la kuhuzunisha ni kwamba baadhi ya wanaume huweza kufika kileleni haraka mno; dakika chache tu baada ya kuingiza uume kwenye uke, ingawa hii humpa mwanaume raha ya ajabu hata hivyo anaweza kumwacha mke wake katika kukatishwa tamaa na kutoridhika hasa kama ni mwanamke ambaye kufika kwake kileleni hutegemea msuguano wa uume kwenye uke wake.

Kawaida mwanaume huweza kuwa tayari kufika kileleni kila baada ya mipigo 50 (kuingiza na kutoka ndani ya uke) na wakati huohuo inachukua zaidi ya dakika 10 kwa mwanamke kufikia kileleni (siyo wanawake wote wengine huwahi).

Mwanaume anapokuwa hana uwezo wa kujizuia kukojoa (ejaculate) mapema huweza kukosa kiwango cha raha ya kutosha anayostahili yeye mwenyewe na mke wake pia, vilevile hukosa raha halisi ya kuwa ndani ya mke wake kwa muda mrefu (mwili mmoja) na hapati zile hisia za ukaribu (intimacy), mapenzi na muunganiko ambao huweza kuwaunganisha wawili wapendanao kupitia tendo takatifu la ndoa ambalo Mungu alilifanyia ubunifu kwa ajili ya mwanaume na mwanamke duniani kuwa pamoja na kufurahia uumbaji wake.
Wanawake wengi huhitaji mume kukaa ndani ya uke kwa muda mrefu unaotosha kwa kadri wanavyohitaji raha na utamu wa hii zawadi ya mwili.
Na njia sahihi ya kuweza kufanikisha hili ni pale tu mwanaume anapokuwa na uwezo wa kuhimili kutokojoa mapema na kuwa na uwezo wa kuwa na hiari wakati gani aweze kukojoa au kutokukojoa.


Fikiria raha inayopatikana kwa mwanaume ambaye anaweza kumhakikishia mpenzi wake anapata raha kwa muda anaoutaka maana tendo la ndoa ni haki yake ya msingi ya kuzaliwa.

Kwa kujifunza unaweza kuwa na uwezo wa kufika muda mrefu vyovyote unataka na kukupa ridhiko la kimapenzi wewe pamoja na mpenzi wako.

Mwanaume anapokuwa kwenye mahaba asipokuwa makini huweza kufika mahali mambo yakawa matamu kiasi kwamba hakuna kurudi nyuma (no point of return) kwa maana kwamba lazima mwanaume akojoe, hana chaguo bali kumaliza hata hivyo kumbuka mke wako ni muhimu pia na mwitikio wa mapenzi kati yako na yeye ni tofauti, ili kumtanguliza yeye unahitaji kufanya kitu nacho ni kuthibiti kutowahi kukojoa kabla yeye hajaridhika.


Habari njema ni kwamba mwanaume yeyote pamoja na wewe unayesoma unaweza kujifunza na kuwa mwanaume anayeweza kufika kileleni wakati anaotaka yeye.
Naamini ni ndoto ya kila mwanaume kuwa mzuri katika mapenzi na kuhakikisha mke wake mpenzi anapata kile anastahili wakiwa faragha na zaidi kuweza kumfikisha mwanamke katika kiwango cha juu kabisa cha raha ya mapenzi ambayo ni ndoto ya binadamu yeyote duniani ambaye ana hisia kamili za kimapenzi.

Saturday, 16 January 2016

SANAA YA MAPENZI.

Mapenzi ni sanaa, huelezea maisha, leo ni tofauti na jana na jinsi binadamu wanafanya mapenzi kufanya mapenzi hubadilika kila siku, mtazamo wa kufanya mapenzi enzi za bibi yako na babu yako ni tofauti na leo.
suala la kufurahia raha ya mapenzi halina mipaka katika ubunifuna huwezi kupima raha ambayo mtu anapata kutokana na kufanya mapenzi.
Huwezi kuweka mapenzi kwenye box au kujenga fence au kuweka mipaka.
Unaweza kuwa na sanaa bora katika mapenzi au sanaa ovyo katika mapenzi.
Unaweza kujidhania wewe ni bora katika sanaa ya mapenzi hata hivyo ukashangaa mpenzi wako hawezi hata kusisimka kutokana na usanifu wako na unaweza kukatishwa tama na kile ulitarajia.

Wakati mwingine unaweza kushangaa jinsi sanaa yako ya mapenzi inavyopata kibali kwa mpenzi wako kama vile maji yanavyotiririka kwenye mto uliozungukwa na ndege wanaoimba sauati ya asili.

Kila mmoja anatakiwa kufungua nafasi yake kupokea raha mpya ya kimapenzi ilimradi unaishi na upo hai.

Je, ni nini siri ya mahusiano (ndoa) yanayodumu na kumfanya mtu aridhike?
-Kuwa na vicheko?
-Kufanya mapenzi?
-Pesa?
-Uaminifu?
-Urafiki?
-Kufanana?
Kila mtu anaweza kuwa na jibu lake hapo.

Friday, 15 January 2016

AJISIKIE VIZURI KWANZA.

Kuna tofauti kubwa sana ya maana na mwitikio wa mapenzi kati ya mwanaume na mwanamke.
Wanaume kawaida wanauwezo wa kutenganisha mwili na moyo.

Kwa upande wa wanawake tunaweza kusema wao wamekomaa kimapenzi kuliko wanaume kwa sababu kwao kutenganisha mwili na moyo inakuwa vigumu na wakati mwingine haiwezekani.
Mwanamke anapompenda mwanaume huanza na hisia za ndani za moyo wake kisha hisia za nje za mwili wake;
wakati mwanaume anapompenda mwanamke huanza kupenda kuanzia hisia za nje za mwilini mwake kisha hisia za ndani za moyo wake.

Ni rahisi mwanaume kukwambia anakupenda kumbe hakupendi bali anakutamani tu na wanawake wamekuwa wanaumizwa sana na wanaume kutokana na hii style yao ya kupenda kwa kumuweka mtu moja kwa moja kwenye moyo wake.

Utafiti mwingi unaonesha kwamba wanawake wengi huwa hawafurahii kufanya mapenzi na mwanaume asiyempenda;
wakati wanaume wanaweza kufurahia na kupata raha ya mapenzi (kufika kileleni) hata kwa mwanamke asiyempenda.
Ndiyo maana mwanaume anaweza kutembea na mwanamke yeyote hata kama ni mbaya kila idara ukilinganisha na mke wake.
Ndiyo maana matukio mengi ya ubakaji hufanywa na wanaume.
Ndiyo maana nyumba ndogo nyingi (wanawake) si wazuri kama nyumba kubwa (wake zao halisi)

Wanaume wanaweza kutenganisha upendo na kufanya mapenzi (love and sex).
Wanawake hutazama kufanya sex ni kitendo cha ziada baada ya upendo wa kweli na wakati mwingine hufanya mapenzi ili kuimarisha mapenzi kwa mwanaume, wakati wanaume sex ni kwa ajili ya kufurahia tu siyo lazima awe anampenda mwanamke anataka kufanya naye sex.

Kwa mwanaume kufanya sex ni kitu kinachofanywa nje ya mwili kwa sababu viungo vyake vya kufanyia vya sex vipo nje na anapofanya mapenzi anakuwa anafanya kitu kwa mtu mwingine (mwanamke) kama vile kupigilia msumari kwenye ukuta;

Kwa upande wa wanawake viungo vya sex vipo ndani ya mwili na kwao kufanya mapenzi ni kama kumkaribisha mtu ndani ya nafasi ya ndani yake, hivyo inakuwa ngumu kutenganisha mwili, moyo na hisia zake.

Kama ilivyo kwa watu wote kwamba mtu mgeni akiingia nyumbani kwako hutajisikia raha kwanza au hutajisikia salama hadi ufahamiane naye, ndivyo wanawake walivyo.Kwa mwanamke kufanya mapenzi na mwanaume asiyemfahamu au mgeni au asiyempenda ni sawa na mtu anayeingilia mipaka ya shamba lake,

Kumvamia mwanamke bila kuonesha upendo wa kweli ni sawa na kuvamia mipaka ya mashamba ya watu, au ni sawa na kuingia kwenye nyumba za watu bila kukaribishwa.
Wanawake hupenda kuwa na ukaribu na upendo wa kweli ili kumruhusu mwanaume kuwa naye kitandani na kuingia kwenye nafasi yake ya siri kufanya mapenzi.Ndiyo maana huwa wanajisikia kutumiwa na kuumizwa na mwanaume ambaye haoneshi upendo wa kweli.

Wanahitaji mwanaume anayewasililiza, anayewapenda, anayewajali, anayekuwa tayari wakati wanamuhitaji, mwanaume anayebembeleza, mwanaume ambaye anajua kuwahudumia wao kama viumbe rasmi na maalumu ambao Mungu ametoa zawadi kwa wanaume duniani.
Hii ndiyo sababu mwanamke hupenda kujisikia vizuri kwanza ili afanye mapenzi wakati mwanaume hujisikia vizuri baada ya kufanya mapenzi.

NI MUHIMU KUMFANYA MUMEO ARIDHIKE..

Kumfanya mume wako aridhike kimapenzi maana yake ni kufanya akuangukie kimapenzi zaidi.
Kufanya mapenzi kwa wanandoa ni njia nzuri ya kuwaunganisha kinafsi na kujipa raha na ukaribu.

Ukijifunza sanaa ya kumkaribisha na kuwa tender kwa mwenzako basi mnaweza kutengeneza bond ambayo ni strong na mume au mke atakufurahia siku zote za maisha yenu.
Kumfanya mwanaume awe na furaha kwa mke wake huonesha jinsi unavyompenda na pia inampa msukumo wa kuhakikisha anakuwa karibu na wewe kimahaba na kuwa na muda na wewe kama wapenzi .
Kuna vitu vingi ambavyo mwanmke huhitaji kufanya kwa mume wake hata hivyo kila mwanaume ana tofauti na mwingine na kila mwanaume ana ladha yake linapokuja suala la mapenzi au tendo la ndoa.

Hivyo ni jukumu la wewe mwanamke kujifunza na zaidi kufanya utafiti wa kutosha kujua mume wako anapenda kitu gani kwako na pia mwili wako upo sensitive wapi.

Kila mwanaume hupenda kuona mke wake akionekana sexy na nguo zile amevaa, inawezekana mpo wawili tu yeye na wewe, kwa nini usimtanie mzee na kinguo cha uhakika kisha pima meter yake itasoma vipi?

Kuna vinguo vya kuogea, kuna vinguo vya chumbani, kuna nguo za kuvaa ofisini au kazini nk kila nguo huvaliwa mahali pake.

*Huwezi kuvaa nguo ya kazini chumbani!

Unajua kuchezesha sauti pia kuna raha yake kumfanya mwanaume joka litoke pangoni, siyo kila siku kulalamika tu, lawama tu, manung’uniko tu, acha hizo jaribu siku hata kama anakosea kila siku anza kumsifia hata kwa vitu vidogo tu, mpe asante, mkumbatie na kumpa romantic touch, uwe mbunifu.

Siamini kama kuna mwanaume ameoa mke ambaye siku zote ni kelele au kununa tu, au kulalamika tu au kuongea tu makosa na kusahihisha, kwa nini asikukwepe, hata kama anakosa siku zingine geuza udhaifu wake kuwa kitu kizuri au uwe na mtazamo positive.

Hata siku moja hujamchezea kifua au kidevu chake, mfanye ajisikie yeye ni mwanaume special.
Mwanamke anatakiwa kumlinda mumewe na maadui wote kiroho na kimwili lakini wakati mwingine mke hujisahau na kuzoea ndoa hadi mume ana fall in love kihisia na mwanamke mwingine (nyumba ndogo).

Hata hivyo inawezekana mume huwa haja fall I love na yule mwanamke bali ame-fall in love na hisia zile wewe humpi na akikutana na huyo mwanamke anajisikia raha na kupata kile love tank yake ndani ya moyo wake huhitaji hata kama mwanamke mwenyewe hampendi ila emotionally ameoza kwa huyo mwanamke na anajikuta anavutwa na yeye badala ya wewe kumvuta.

NI KATIKA AFYA NA UGONJWA..

Ndoa ni kazi na wakati mwingine huweza kuwa kazi nzito na ya ziada.
Watu wengi hukumbana na wakati mgumu kwenye ndoa wakati fulani inawezekana hata wewe upo kwenye wakati mgumu sana wa ndoa yako, hata hivyo swali gumu ambalo linahitaji majibu ni
je, mume wako au mke wako anapokuwa amepata tatizo kubwa la kiafya kwa mfano hawezi kushiriki tendo la ndoa na wewe, hawezi kula mwenyewe, ameharibika sura kwa sababu ya ugonjwa au inabidi umbebe kwa ajili ya haja zote ndogo na kubwa,

Je, utakimbia?, utakaa naye?,
utamuomba Mungu?
Utaomba talaka?

Utakimbilia kwenye kifua cha mwanaume au mwanamke mwingine?

Au ndo wakati wako wa kujirusha?

Unaweza kuangalia maswali hayo na kujiuliza
“hivi ni nani anaweza kufikiria kufanya vitu kama hivyo?”

Ukweli kuna mifano hai ambapo baada ya mmoja ya wanandoa afya kuzolota mwingine amefanya moja ya hayo hapo juu.

Wakati wanandoa wapo mbele ya kanisa na mbele ya mchungaji, kutoa viapo vyao mara nyingi ni rahisi sana kusema

“katika afya au ugonjwa nakubali”
au
‘Katika utajiri na umaskini nakubali”,

Wakati wote mna afya njema ni rahisi sana kukubali lakini wakati ukifika umaskini ukaanza kuwakalia kwa kasi ya ajabu, au mmoja afya kuzolota ndipo unaweza kukumbuka kile kiapo kilikuwa kina maana gani.

“Moyo wangu ulikufa ganzi pale niliposikia mume wangu mpenzi ana Cancer na ipo hatua ya 4 ambayo hakuna dawa duniani.
Hadi hapa tulikuwa wanandoa wazuri na wenye raha pamoja na watoto wetu na tulipenda na kila mmoja kujisikia raha kwa mwenzake.
Mume wangu mpenzi alianza kuugua alianza kupunguza uwezo wa kwenda kufanya kazi kila siku hadi ikafika siku hawezi kula chakula mwenyewe hadi nimlishe huku amelazwa Hospitalini.
Wengine waliona ni udhaifu wa mume wangu kshindwa hata kula mwenyewe ila mimi nilimuona jinsi anavyojitahidi kutumia nguvu zake na ilishindikana, niliona anavyoteseka kwa maumivu hadi nikamuomba Mungu anipe nguvu kuvumilia kuona mume wangu katika ugonjwa namna hii.
Ilibaki mimi kuwa pembeni kwake usiku na mchana na kumuonesha mume wangu upendo mkuu na kwamba bado namuhitaji kuliko wakati mwingine hata kama alikuwa kwenye kitanda cha mgonjwa, Mungu aliniwezesha kunipa nguvu na ujasiri kuendelea kumuona mume wangu bado ni mume wangu hata kama alikuwa amebadilika sana kwa jinsi ugonjwa ulivyomharibu.

Ili niweze kupita katika haya yote nilikuwa namuomba Mungu ili niwe strong na anilinde kupita katikati ya kipindi hicho kigumu na Mungu alinionesha njia ya kumsaidia mume wangu na njia pekee ilikuwa ni mimi kuendelea kumhudumia “Kama Mume wangu” bila kujali alikuwa katika hali gani.
Alikuwa anaongea mama mmoja kwa uchungu na moyo wa machozi kuonesha kwamba kweli ndoa ni kujitoa na alikuwa anajua kuwepo wakati mumewe afya imezolota".

Swali Je utakuwa pamoja na mume wake au mke wako akiwa katika ugonjwa?

Jibu ni
Endelea kumpenda kama ulivyokuwa unampenda
Omba Mungu akupe uwezo na nguvu na uvumilivu,
Uwe pamoja na yeye,
Usikimbie,
Usikate tamaa,
Simama na toa upendo wako maalumu na
Mpende mpende na endelea kumpenda.

Thursday, 14 January 2016

WANAPENDA MUWE HIVI KITANDANI..

Kila mwanamke huwa na ndoto za kufanikiwa maisha;
kuwa na familia, kuwa na mume ambaye atampenda maisha yake yote nk.
Ni hakika wanawake ni tofauti na wanaume, inawezekana hilo umelijua, kuna mambo ambayo wanaume hufanya kitandani na kumfanya mwanamke ajione ni mwenye furaha duniani na pia kuna wakati kuna mambo yanafanywa na wanaume kitandani na hupelekea mwanamke kujuta na kuumizwa hisia zake.

Mambo yafuatayo ni muhimu sana kuzingatiwa na mwanaume akiwa chumbani kwani wanawake wengi wanakiri kwamba mambo madogo kama haya wakati mwingine huwafanya kujisikia vibaya hasa linapokuja suala la mahaba.

1.USAFI
Kuwa msafi ni msingi wa mambo yote kitandani, ni vizuri kuoga kabla ya kulala hata kama kuna matatizo ya maji lazima uweke bajeti yako vizuri kuhakikisha unaoga kabla ya kurukia kitandani.
Usafi ni pamoja na sehemu zote za mwili wako, mikono safi na kucha zilizopunguzwa vizuri, pia kunyoa ndevu vizuri, kuna wakati kidevu kikigusa mwili wa mwanamke humkwaruza na kumuumiza, labda uwe na mke anayependa kidevu kama kile cha Osama.
Pia wapo wanaume ambao huvuta sigara na bila kuwa makini huingia chumbani na harufu ya sigara huku midomo inanuka, hapo unaharibu kila kitu.

2.KUWEPO
Ni vizuri kuwepo kwenye tendo lenyewe na mhusika mwenyewe kiroho, kimwili na kiakili, kama upo kwenye tendo la ndoa mwanamke hujisikia vizuri kwa kuwa utashirikiana na mwanamke kwa kila hatua na atajiona ni sehemu ya utendaji.
Tamka jina lake, tamka maneno mazuri na kuonekana upo na yeye isiwe kama vile wewe upo na mashine fulani ya kukupa raha.
Pia wapo ambao anaanza then anaacha (anajibrekisha), mwanamke ni tofauti na mwanaume hivyo basi kama utaacha ujue lazima ukaanze upya.
Pia wapo wanaume wanajua kabisa mwanamke ni umbo dogo na yeye mwanaume ni umbo kubwa, sasa ukimlalia na kuendelea na shughuli bila kujua hapo chini anaendeleaje si anaweza akashindwa hata kupumua, wewe kuwepo ni pamoja na kujua na kumsoma anauonaje muziki wenyewe.

3.MAANDALIZI HUANZA TANGU NGUO ZIMEVALIWA.
Mwanaume unahitaji kuanza kumuandaa mwanamke tangu mapema (kisaokolojia) tangu asubuhi mnaamka, mchana kwa kuwasiliana, jioni kwa kuwa pamoja, then chumbani ni mahali ambapo mnamalizia mission ya siku nzima tena kwa kila mmoja kumvua mwenzake nguo.
Kuna raha mtu kubaki na nguo za ndani tu, na pia kuna raha kuwa naked, kila kitu kina raha yake.

4.KUFANYA VILEVILE NA KUACHANA NA SEHEMU ZINGINE ZA MWILI WAKE
Uwe makini kuangukia kwenye utaratibu wa ratiba ya kila siku kitu kilekile wimbo uleule, mziki ule ule na mwimbaji yuleyule.
Una mbusu, unachezea matiti then penetration, huna time hadi chumbani?
Ukifanya hivi kwa kuzoea basi mwanamke atajisikia bored.
Unahitaji kuwa mbunifu na mtundu kujua sehemu zingine ambazo anaweza kusisimka na ukampa utamu mpya wa tofauti.
Even an old dog can learn new tricks.
Na kuna wengine hata kukiss hakuna kila siku yeye ni kurukia tu.

5.KUWA BUBU
Hata kama wewe ni bubu naturally linapokuja suala la mahaba unahitaji kuongea lugha unayoijua wewe ambayo itaonesha unampa appreciation kwa juhudi ambayo mke wako anafanya wakati wa tendo la ndoa.
Kama anakuuliza au anakuomba uwe unaongea ni vizuri sana ukawa unaongea wakati wa mahaba kwani kuna raha yake na utamu wake.

Kumbuka kwamba mwanamke kuathirika sana na maneno ambayo mwanaume anaongea ndiyo maana linapokuja suala la kudanganywa wanawake wengi (si wote) ni rahisi sana, hivyo basi mwanaume anayeongea wakati wa mahaba ana raha yake kwa mwanamke.
Ila uwe na kiasi usiwe unaongea tu kama radio.
Pia kuna wanawake huwa wanapenda kusikia dirty words na wengine hawapendi kabisa so uwe makini na mke wako kama anapenda mpe na kama hapendi achana kabisa.

6.KUCHEZA RAFU
Uwe mstaarabu kwani tendo la ndoa si vita.
Hakuna mwanamke anapenda matiti yake yachezewe ovyo kwa kunyumbuliwa huko na huko kama vile unataka kuyanyofoa, pia chuchu zisibonyezwe kama vile unafungua radio,so ubonyeza tu hadi radio ikome, fanya taraatibu, pia hata kama anakuruhusu upeleke mkono wako hapo chini basi fanya kila kitu kwa uangalifu ili usimuumize.
Kama unafanya vizuri utajua na kama anahitaji mgandamizo zaidi (pressure) atakwambia hata kama ni aina ya mwanamke anayependa rough sex atakwambia tu, kwani mambo ya sex ni ya ajabu sana na yana vituko vya kila aina.
Hujasikia watu wanatukana matusi mazito wakifika kileleni?
Pia wapo ambao hufanya kama vile wapo kwenye mbio za Olympic na kujaza kama vile kuna mashindano ya hydraulic mashines.
Fanya kwa taratibu na wote mtapata utamu zaidi.

7.KUMALIZA MAPEMA
Kama ni mwanaume ambaye unamaliza mapema ni muhimu kuchukua tahadhari na kujifunza jinsi ya kuchelewa kumaliza mapema kwani mara nyingi mwanaume akimaliza mapema mwanamke hukatizwa utamu na anakuwa hana jinsi.
Ni vizuri kutumia utundu wako kumfikisha kileleni yeye kwanza kabla yako.

8.KUCHELEWA KUMALIZA
Wapo wanaume ambao hubaki wamedinda masaa na wakati huohuo mke amesharidhika, kitu ambacho hupelekea mchezo mzima kuwa gwaride na mwanamke humalizwa energy na kuanza kutokuwa na hamu ya tendo kila akikumbuka urefu wa gwaride alilopewa.
Ni vizuri kuwa makini kusoma saikolojia na mwendo wa tendo lenyewe ili kujua gia unayotakiwa kuweka ili kufika pamoja katika kituo cha basi kinachotakiwa.

8.KUTOKUSHUKURU
Mwanamke anahitaji kupewa credits kwa kazi aliyofanya, unahitaji kumshukuru, sema asante kwa hudumu yake na ili uwe mwanzo wa huduma nyingine bora zaidi.
Hujasikia tendo la ndoa ni dawa, na kama ni dawa maana yake amekupa tiba ndiyo maana hata ukiwa kazini unachangamka kwa sababu unapata kitu kizuri kwa mke wako, hivyo anastahili kupewa asante.